Baada ya kukupa Tip#2 kwamba kila kijana anapaswa kuelewa umuhimu wa Kujithamini (Self-esteem) na Kujiamini (Confidence) na kuwa mambo haya mawili yanaweza kumjenga na kumbomoa mtu. Ukosefu wa kujithamini na kujiamini ndo mwanzo wa kuporomoka kwa mafanikio yako, tulikudokeza mbinu ya kuanzia ni kujiwekea nafsi yako katika mtazamo wa juu (positive self-talk).

Sauti inayosikikia ndani ya kichwa chako ina uwezo wa kukufanya ujithamini kwa hali ya juu katika kila hatua unayochukua kwenye mambo yako. Watu maarufu na wenye mafanikio kimataifa, mfano Oprah, Jay Z, Usain Bolt, Patrick Ngowi na wengine wengi wamekiri kuwa wanayo tabia ya ‘positive self-talk’ kwa muda mrefu sana.

Watu wenye mtazamo HASI hawaachi kulalamika hovyo, kila kitu wao hukichukulia negative. Ni wagumu kuji ‘adapt’ na hali halisi, hawana subira na hupenda kuponda kila mtu au kila kitu. Muda wao mwingi hupoteza katika kuwaza mambo yasiyoweza kuwasaidia chochote. Mara nyingi hujiangusha wenyewe kwa kuwa na mtazamo HASI na tabia ya ‘negative self-talk’. Tuangalie mambo yanayoendelea kichwani mwako, kama wewe ni katika kundi la watu wasiojiamini wala kujithamini;

- Una imani kuwa wewe hauko sawa kama mtu wa kawaida

- Unajisikia hovyo, mpweke na stress zimekujaa ndani yako

- Unajiona una mapungufu mengi mfano, mtu akikusifia “umependeza”, badala ya kusema “asante”, huku ukitabasamu, jibu lako huwa “aaah kupendeza nitapendeza mie bwana, nguo yenyewe mtumba na sura yenyewe hii kama…...”

- Unajiona kuwa thamani yako ni ndogo, mfano “mimi sifai”, “mimi mjinga – sina akili”, “kila mara nashindwa au nafeli”.

- Una mtazamo hasi juu yako binafsi na uwezo wako wa kutimiza malengo uliyojipangia, mfano –“sidhani kama nitaweza kufanikiwa hilo….” “Mimi siwezi bwana….” “Aaaah hiyo haiwezekani, haiwezi kufanya kazi”.

- Unapoteza kujiamini kwako na unaona ‘future’ ya mbele hakuna kitakachobadilika

- Una imani ndogo sana kwa vitu vilivyoko maishani mwako

- Una amini kuwa ulimwengu hauwezi kukutimizia mahitaji yako binafsi

- Una acha kujishughulisha katika kuhangaika kutimiza ndoto zako

- Unagundua kuwa huna furaha wala mafanikio kama watu wengine walio fanikiwa

- Unaona watu wengine kuwa ni bora zaidi, wenye nguvu na wana mafanikio kuliko wewe. Unawaacha wakutumie au wakusaidie mambo yako

- Unaumia chinichini, unasononeka au unasikitishwa na hao watu

- Unajiona wa hovyo, au usiye kuwa na shukrani kuwa na mawazo ya hivyo kwa hao watu

- Unajisemesha mwenyewe na kujinyamazisha. Unajiadhibu kwa kushindwa kuwa kama wengine

- Unapojitazama, unajiona kama unatumiwa na wengine ili wajinufaishe mahitaji yao

- Unajijengea kichwani mwako imani ya nguvu zaidi kuwa wewe sio mtu sawa, tena una kasoro

- Unaachana kabisa na swala zima la kujithamini na kila kukicha mambo hayo hapo juu yanajirudia upya tena na tena

Tuangalie sasa hii tabia ya kutokujithamini (negative self-talk) ina anzaje anzaje!

- Kuna baadhi ya matukio yaliyokukuta maishani mwako yanaweza kuwa chanzo cha kukuletea hali ya kutokujithamini (low self-esteem) katika maisha yako.

- Kushushwa thamani mara nyingi na kudhalilishwa – hii inaweza kutokea nyumbani, kazini, shuleni, au popote pale

- Kubeba lawama ya vitu ambavyo hujahusika wala sio kosa lako

- Kukosekana kwa kutimiziwa mahitaji yako ya msingi

- Kudhalilishwa au kuteswa, mfano mtoto kutukanwa sana au kupigwa hovyo

- Kufanyiwa udhalilishaji au mateso ya aina nyingine, mfano kubakwa au kubaguliwa

- Kuwa na "label" iliyogandishwa kwako na watu wengine, mfano mlemavu au kuambiwa una wazimu na akili zako haziko sawa

- Kupata ujumbe wa mara kwa mara kuhusu nini wazazi, walimu, n.k.. wanategemea kutoka kwako – hili linaweza kuwa tatizo zito sana kwa watu ambao mzazi wake ni mlevi

- Vitu vinavyo onyeshwa kwenye TV, Movie na matangazo ya biashara yanayo onyesha ni kitu gani kinachotarajiwa kutoka kwako na unatakiwa uwe vipi, kimaumbilie, kimavazi na kazi nzuri yenye status

Hivi ni baadhi tu ya vitu hatuwezi kuviorodhesha vyote ambavyo vina nguvu kubwa sana katika kukubomoa ‘self-esteem’ yako. Hivi vitu vinachangia katika kushusha thamani ya mtu na sio kosa lako. Vinaweza kuwa ni mambo mtu mwingine amekufanyia au jinsi mambo yalivyo katika mazingira unayoishi au uliyokulia.

Huna uwezo wa kumbadilisha mtu. Ila unao uwezo mkubwa wa kujilea, kujitunza, kujibembeleza, kujidekeza, kujipenda na kujipongeza mwenyewe na nafsi yako. Kizuri zaidi ni kuwa unayo ‘control’ KUBWA sana katika kucheza na fikra zako, mtazamo wako ndio silaha kubwa sana ya kukujenga, jinsi utakavyo ‘think’, kujisikia na kufanya kwenye maisha yako. Anza leo KUFUTA fikra zote mbaya (hasi) kichwani mwako, jaza positive things na utaanza kuona hali ya maisha yako inavyobadilika.

Tembelea ukurasa wetu kesho tukijaaliwa tutazungumzia jinsi utakavyo jikuta kwenye dimbwi la moto kama utashindwa kuachana na ‘negative thoughts’. Amini usiamini, mitizamo HASI na mambo yanayosikika kichwani mwako ni hali inayoweza kukubomoa. Tutakupa mbinu zingine zitakazokusaidia katika kujijengea tabia za kujiamini na kuachana na mawazo HASI ya kujishusha thamani. Tunakutakia siku njema!

kwa hisani y shear illusion

Categories:

Leave a Reply